Huduma ya
Maombi na Ushauri
MAOMBI
Huduma za maombi ndizo msingi wa huduma ya World Healing. Kanisa linaamini katika nguvu ya maombi kama njia ya kuwasiliana na Mungu na kufungua milango ya uponyaji, ukombozi na mafanikio.

Maombi ya Kila Wiki
Kanisa huendesha ibada za maombi kila wiki zenye lengo la kujenga imani na kuimarisha maisha ya kiroho ya waumini.

Maombi ya Uponyaji
Waumini na watu wanaotafuta msaada wa kiroho hukaribishwa kupokea maombezi kwa ajili ya uponyaji wa magonjwa ya mwili, akili na roho.

Maombi ya Timu
Timu maalum ya waombezi hujitolea kuombea familia, jamii, taifa na makanisa mengine kwa ajili ya amani, mafanikio na uvuvio wa kiroho.

Maombi Maalumu
Kanisa huandaa makesha na makambi ya maombi mara kwa mara, ambapo waumini huombewa maono na mwelekeo wa maisha yao
USHAURI
Huduma ya Ushauri

