Ibada Zetu
KARIBU KWENYE IBADA ZA
World Healing Church
Tunapenda kukualika kwa moyo mkunjufu kwenye Ibada zetu za Jumapili, Jumatano na Ijumaa katika Kanisa la World Healing – kanisa lililojengwa juu ya msingi wa Injili safi ya Yesu Kristo, likiwa na kusudi la kubadilisha maisha kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu.
Ibada ya Jumapili
Ibada ya Jumapili ni Ibada ya furaha kuu kwa familia ya World Healing! Ni wakati wa kukusanyika kama mwili wa Kristo kumpa Mungu sifa, kuabudu kwa unyenyekevu na kupokea neno la uzima linalobadilisha maisha.
Ibada ya Jumapili inahusisha:
Sifa za nguvu na zenye upako:
Tunamwimbia Bwana kwa shangwe na furaha, tukimkiri kuwa mkuu juu ya yote.
Kuabudu kwa undani:
Tunainua mioyo yetu mbele za Mungu kwa nyimbo za ibada zinazoleta uwepo wa Mungu wa kipekee.
Neno la Mungu la kina na la kinabii:
Mchungaji na watumishi waliopakwa mafuta huleta ujumbe wenye kuelekeza, kufariji, na kutia nguvu kwa maisha ya kila siku.
Maombezi na huduma binafsi:
Baada ya neno, kuna nafasi ya kupokea maombi kwa ajili ya uponyaji, ukombozi, na msaada wa kiroho.
Ibada ya Jumatano
Ibada ya Jumatano ni ya wanafunzi wa kweli wa Kristo – wale wanaotamani kulielewa Neno kwa undani na kulionyesha katika maisha ya kila siku.
Katika ibada hii:
- Tunachambua Maandiko kwa mtazamo wa kiroho na wa vitendo.
- Tunajifunza namna ya kuyatekeleza mafundisho ya Kristo katika ndoa, kazi, familia na huduma.
- Kuna majadiliano ya wazi, maswali na majibu, na mafundisho ya kina kutoka kwa watumishi wa Mungu waliobobea.
Muda wa Ibada :
SAA 11:00 JIONI
Tutembelee :
Sheli ya Kwalala,
Barabara ya Old Moshi
Kijenge ya Chini, Arusha
Ibada ya Ijumaa
Ijumaa ni siku ya vita vya kiroho na kuvunja minyororo ya giza! Huduma hii ni maalum kwa maombi ya nguvu, maombezi, na ukombozi kwa kila eneo la maisha.
Unapohudhuria:
- Utajifunza namna ya kuomba kwa ushindi.
- Utashirikiana na waombaji wengine kuombea familia zako, kazi, afya, na ndoto zako.
- Ni wakati wa kupokea moto wa maombi, neema ya kushinda vikwazo, na msaada wa ki-Mungu kwa mapambano ya maisha.
Muda wa Ibada :
SAA 11:00 JIONI
Tutembelee :
Sheli ya Kwalala,
Barabara ya Old Moshi
Kijenge ya Chini, Arusha
Usikose nafasi ya kuonja uwepo wa Mungu, kusikia sauti Yake, na kuanza safari mpya ya kiroho yenye uzima wa milele. Hakika utasema, “Hakuna kama Bwana wetu!”

