KARIBU
World Healing Church
“Imani Inaachia Nguvu”
Kanisa la World Healing ni huduma ya Kikristo iliyojikita katika urithi wa kiroho Afrika. Tumejitolea kutangaza Injili ya Yesu Kristo, kubadilisha maisha, na kuinua ustawi wa jamii za Kiafrika na kwingineko kupitia nguvu za Roho Mtakatifu. Kwa njia ya ibada na uinjilisti, uanafunzi, na huduma za kiutu, tunatangaza upendo wa Mungu kwa watu wa asili zote.
Dhamira yetu ni kuhubiri Injili, kufanya wanafunzi, na kuhudumia jamii zenye uhitaji kupitia nguvu ya Injili ili kuwa na ulimwengu uliyobadilishwa ambapo kila mtu anapata upendo wa Kristo na anaishi kwa matumaini, heshima, na kusudi la Mungu.
HUDUMA ZETU
Maombi
Maombi ndiyo msingi wa Kanisa la Word Healing. Tunaamini katika nguvu ya maombi kuwa ni njia ya kuwasiliana na Mungu na kufungua milango ya uponyaji na ukombozi.
Umisheni
Umisheni ni moyo wa huduma ya Kanisa la World Healing, ikiwa ni agizo kuu la Yesu Kristo kwa kanisa lake. Huduma hii mi kwa ajili ya kuwafikia walio mbali na neno la Mungu
Jamii
World Healing Church haitenganishi huduma ya kiroho na mahitaji ya kimwili ya jamii. Kupitia huduma za kijamii, kanisa linatekeleza upendo wa Kristo kwa watu wote.
IBADA ZETU
Msingi wa huduma yetu ni ibada zinazoongozwa na Roho Mtakatifu, zinazobadilisha maisha, maombi yenye nguvu, na mafundisho yenye matokeo yanayojikita katika Neno la Mungu.
Ibada ya Jumapili
SAA 4:00 ASUBUHI
Ibada ya kumpa Mungu sifa, kuabudu kwa unyenyekevu na kupokea neno la uzima linalobadilisha maisha.
Ibada za Jumatano
SAA 10:00 JIONI
Ikiwa unatamani kulielewa Neno kwa undani na kulionyesha katika maisha ya kila siku, karibu kwenye Ibada hii.
Ibada za Ijumaa
SAA 10:00 JIONI
Ibada ya vita vya kiroho na kuvunja minyororo ya giza, maombi, maombezi, na ukombozi kwa kila eneo la maisha.

